KUCHUNGUZA UJENZI WA DHAMIRA ZA METHALI KATIKA DIWANI YA SAADANI KANDORO KATIKA MUKTADHA WA JAMII YA KISASA
DOI:
https://doi.org/10.51984/johs.v24i2.3582Keywords:
Diwani, Methali, Dhamira, Jamii ya kisasa, Muktadha wa jamii ya kisasaAbstract
Wimbi la sayansi na teknolojia limezikumba jamii nyingi, ikiwepo jamii ya Waswahili. Wimbi hili limezifanya jamii kueleza fikra na mitazamo yao kwa njia ya kijigitali jambo ambalo linachochea mabadiliko ya matumizi ya lugha. Katika muktadha huu methali kama sehemu ya hazina ya fasihi simulizi zinakabiliwa na hatari ya kusahauliwa na kupuuzwa, hasa, na kizazi kipya ambacho ndicho kilichokumbatia zaidi usasa katika mawasiliano na burudani. Pamoja na changamoto hizo, methali bado zinaendelea kuwa ni ghala muhimu lenye kuhifadhi ukweli wa maisha, elimu, maadili na utamaduni wa kijamii. Hivyo basi kazi hii inachunguza ujenzi wa dhamira za methali katika diwani ya Saadani Kandoro katika muktadha wa jamii ya kisasa. Methali, kama sehemu ya urithi wa fasihi na utamaduni wa Kiswahili, zimekuwa na nafasi muhimu katika kuendeleza maadili, mitazamo ya kijamii, na mshikamano wa jamii kwa miongo mingi. Hata hivyo, katika zama za sasa zinazokumbwa na mabadiliko ya kijamii, kiteknolojia na kiutamaduni, matumizi na tafsiri ya methali yanahitaji kuchunguzwa kwa mtazamo mpya. Utafiti huu ulitumia mbinu ya uchanganuzi wa kijamii wa fasihi (sociological literary analysis) kuchambua methali zilizotumika katika mashairi ya Kandoro. Methali 19 ziliteuliwa na kuchambuliwa kwa kuzingatia mchango wake katika kujenga dhamira zinazohusiana na maisha ya jamii ya sasa. Nadharia ya kijamii ya fasihi ilitumika kufafanua namna methali hizi zinavyowasilisha mitazamo ya kijamii, mabadiliko ya maadili, haki, usawa wa kijinsia, na mshikamano wa kijamii. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa methali katika diwani ya Kandoro bado zina nafasi muhimu katika jamii ya sasa. Methali hizi hutumika kuhamasisha maadili bora, mshikamano wa kijamii, heshima ya binadamu, na haki za kijamii. Aidha, zimejipenyeza katika mawasiliano ya kisasa kupitia majukwaa ya mitandao ya kijamii, memes, na mijadala ya mtandaoni, hivyo kuendelea kuathiri fikra na mitazamo ya kizazi kipya. Kwa ujumla, utafiti huu umebainisha kuwa methali si tu urithi wa kale bali ni zana hai ya kufundisha, kuonya na kuhamasisha jamii katika zama za sasa. Utafiti unapendekeza kuendelezwa kwa matumizi ya methali katika elimu, fasihi, na mawasiliano ya kijamii ili kusaidia kukuza jamii yenye maadili, mshikamano, na heshima kwa utu wa binadamu.
Downloads
Downloads
Published
License
Journal of Humanities Policy on Intellectual Property and Plagiarism
1. Commitment to Intellectual Property and Ethics
The Journal of Humanities (JOHS) is fully committed to respecting intellectual property rights and aims to protect the originality and authentic work of authors who submit their manuscripts for publication. The journal takes a firm stand against articles that contain any form of plagiarism and emphasizes the need for all researchers to adhere to the highest ethical standards in scientific research.
2. Anti-Plagiarism Policy
The journal considers plagiarism a serious violation of academic ethics. Therefore, authors must ensure that their work is original and not plagiarized, and that any use of external sources is properly cited and documented according to correct academic standards.
-
Actions Taken: In the event that any plagiarism or academic theft is discovered in a submitted article, the editorial board will contact the author to request a formal explanation within a maximum period of two weeks from the date of notification.
-
Investigation and Decision: After receiving the explanation, the article will be referred to the journal's specialized committees, which will investigate the matter and take the necessary measures, which may include the permanent rejection of the article and the imposition of disciplinary actions.
3. Publication License and Author Rights
The journal adopts the Creative Commons license type Attribution-NonCommercial-NoDerivs 4.0 International (CC BY-NC-ND 4.0), which allows for the following:
-
Attribution: Users are entitled to cite the content published in the journal and use it in their work, provided that the original source and author are clearly credited.
-
Non-Commercial: The published content may not be used for any commercial purpose.
-
NoDerivs: It is not permitted to make any modifications, distortions, or to build derivative works from the published content.
Under this license, authors are required to complete an exclusive license agreement for the journal. Authors retain the rights to their research data and may reuse and share their work for scientific purposes with proper citation.


